Quantcast
Channel: saluti5
Viewing all 8805 articles
Browse latest View live

MZEE MSISIRI ADAI ROHO MBAYA, USHIRIKINA NI VIKWAZO VYA MAENDELEO YA FILAMU BONGO

$
0
0


MKONGWE na nguli wa filamu za kitamaduni, Fadhili Msisiri, ameendelea kuthibitisha kuwa, roho mbaya na imani za kishirikina, ni kati ya vikwazo vya maendeleo katika sana ya filamu hapa Bongo.
Akiongea na Saluti5, Msisiri alisema kuwa, wasanii wengi wa filamu hapa nchini wamekuwa ni watu wasiopenda maendeleo ya mwingine, huku baadhi yao wakiwa tayari hata kwenda kwa waganga ili kuwarudisha nyuma wenzi wao kimaendeleo.
“Utakuta msanii anaandaa filamu na kuacha kumpa shavu yule mwenye uwezo kwa hofu ya kumpandisha chati zaidi na kumfunika, ambapo badala yake humtafuta msanii wa kawaida na kumchezesha, bila kujali kuwa anaishusha kiwango muvi yake,” alisema Msoisiri.
Msisiri alisema kuwa, umefika wakati sasa kwa wasanii wote kuwa kitu kimoja na kupenda kushirikiana, ili kuipandisha juu zaidi sanaa ya filamu, badala ya kukazania kubaniana pamoja na kujawa na imani za kishirikina.

PROSPER: ANGELA OKORIE NI NI KATI YA WANAWAKE WEZI WA KUTISHA DUNIANI

$
0
0


MSANII wa Nollywood, Angela Okorie, anaendelea na maisha na mumewe Prince Ekeh, lakini kesi yake ya wizi ingali inaunguruma mahakamani.
Mpenzi wake wa zamani, Prosper ambaye pia ni msanii wa Nollywood lakini raia wa Afrika Kusini, amesisitiza kuwa Okorie ni kati ya wanawake wezi wa kutisha duniani.
Prosper amepinga madai ya Angela kuwa anampakazia baada ya kuona ameolewa, akasisitiza kuwa anachokitaka ni kurudishiwa fedha zake au ngela akiri kumuibia ili afute kesi mahakamani.

DE GEA KWENYE MTIHANI MZITO, REAL MADRID KULIANZISHA TENA

$
0
0

WAKATI Manchester United wakionekana kutaka kutulia na kuelekeza nguvu kwenye mipango ya kujiimarisha zaidi,  Real Madrid inaanza kuwachanganya.

Kuelekea dirisha la usajili wa Januari, klabu hiyo imeanza tena kusambaza fitna na sumu mbaya kwa kusema itamsajili kipa David De Gea, katika dirisha hilo la usajili.

Taarifa hizo ni mbaya mno masikioni mwa mashabiki wa United kutokana na umuhimnu wa kipa huyo aliye chaguo la kwanza.

De Gea ambae alikwama kuihama timu hiyo katika siku ya mwisho ya usajili wa kiangazi kutokana na kilichoelezwa kuwa ni uzembe, alishabainisha kuwa ana mapenzi na Real Madrid.

Kocha Louis Van Gaal, alishamruhusu kipa huyo kuhama, lakini baada ya dili hilo kushindikana alimsihi arejeshe moyo na kuitumikia United.

Taarifa za Real Madrid zimetiwa nguvu na rais wa Ligi Kuu ya Hispania ‘La Liga’, Javier Tebas ambae alinukuliwa juzi, alisema anaziona dalili za De Gea kukipiga katika Ligi hiyo.

“Sio siri, ingawa De Gea amesaini mkataba mpya wa kuitumikia Manchester United, bado sidhani kama hiyo itafanya abaki huko milele,” alisema.

Aliongeza kusema, kila klabu inahitaji kuwa na kipa bora kama David De Gea, lakini kutokana na ukweli kuwa uyo ni mzaliwa wa Hispania, basi ana nafasi kubwa ya kukipiga nchini humo.

Aliifagilia La Liga akisema ni moja ya Ligi bora zaidi Ulaya katika miaka hii na ushahidi ni jinsi klabu za nchi hiyo zinavyotawala soka la michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya na Europe League.

Aliongeza kusema kuwa, hajali iwapo kipa uyo atachelewa kurudi Hispania, lakini alicho na matumaini nacho ni kuwa, hata De Gea mwenyewe anatamani sana kuanza kukipiga katika Ligi hiyo.

VAN GAAL ADHAMIRIA KUSAJILI WINGA MANCHESTER UNITED

$
0
0

KOCHA mkuu wa Manchester United, Louis Vann Gaal amesema kuwa anataka kusajili winga.

Vaan Gaal alisema kuwa ameamua kufanya hivyo bada ya kugundua baadhi ya kasoro kwenye kikosi chake.

Alisema ameamua kuwafuatilia baadhi ya wachezaji wenye kucheza nafasi hiyo ili kuongeza nguvu katika timu yake mwanzoni mwa mwaka ujao.

“Sitaki kufanya makosa kipindi cha usajili dirisha dogo, nitasajili winga kwa aili ya kuongeza kasi ya ushambuliaji, nimeona kidogo ina kasoro,” alisema.

ZIDANE ASEMA EDEN HAZARD NI WA 'LEVO' YA MESSI NA RONALDO

$
0
0

Gwiji wa zamani wa Real Madrid, Zinedine Zidane, ametoboa siri kwamba uwezo wa mshambuliaji wa Chelsea, Eden Hazard ni mkubwa sana kiasi kwamba anastahili kula sahani moja na Lionel Messi na Cristiano Ronaldo.

Zidane alilieleza gazeti moja la nchini Hispania kwamba anavutiwa sana na uwezo wa mchezai huyo kwa muda mrefu na anatamani siku moja amuone katika kikosi cha Madrid. 

“Hazard naona ana uwezo mkubwa kama walivyo Lionel Messi na Cristiano Ronaldo, ni mchezaji mzuri mwenye kasi na uwezo wa kufunga mabao,” alisema.

Kutokana na sifa hizo, Zidane amesisitiza kuwa ni vema viongozi wa Real Madrid wakafanya kazi ya kumnasa Eden Hazard.

JOSE MOURINHO AAMUA KUMSAJI MKONGWE WESLEY SNEIJDER ....Saido Berahino naye mbioni kutua Chelsea

$
0
0

BAADA ya mambo kwenda kombo, kocha wa Chelsea, Jose Mourinho amedhamria kumsajili kiungo mkongwe Wesley Sneijder raia wa Uholanzi, ili kuokoa jahazi linaloelekea kuzama.

Mourinho amesikia ushauri wa wataalam kuwa timu haina wakongwe wenye hamasa na uwezo binafsi wa kuisaidia timu kama alivyokuwa Didier Drogba.

Kutokana na hilo, katika usajili wa dirisha dogo la Januari, jina la Sneijder linatarajiwa kuwa miongoni mwa majina yatakayotengewa fungu la fedha Chelsea.

Imefichuliwa kuwa, mbali ya kiungo huyo, pia Mourinho anafikiria kumsajili mshambuliaji chipukizi wa West Bromwich Albion, Saido Berahino, mwenye miaka 22.

Fungu la mchezaji huyo kwa mujibu wa klabu yake, ni paundi mil 20, ambazo kwa Chelsea sio kikwazo.

Pia imeelezwa kuwa Chelsea imeshawazidi kete Manchester United katika mbio za kumsajili winga wa Valencia ya Hispania raia wa Algeria, Sofiane Feghouli mwenye miaka 25.

KUBWA KULIKO!! TWANGA PEPETA NA MAPACHA WATATU WAJA NA “USIKU WA KUACHWA” NOVEMBA 28 MANGO GARDEN …Chaz Baba ndani ya nyumba

$
0
0

Ukisikia vitu adimu ndo kama hivi. Hebu pata picha panakuaje pale anaposimama Chaz Baba, Khalid Chokoraa, Kalala Jr na Jose Mara kwenye jukwaa moja huku wakisindikizwa na bendi za Twanga Pepeta na Mapacha Watatu.

Hiyo ni show itakayokwenda kwa jina la “Usiku wa Kuachwa” itakofanyika Mango Garden Kinondoni, Jumamosi hii ya Novemba 28.

Wenyeji wa onyesho hilo – Twanga Pepeta wakiwa wamewaalika Mapacha Watatu sambamba na Chaz Baba kutoka Mashujaa Band, watawakumbusha mashabiki wa muziki wa dansi na hata bongo fleva, enzi za wimbo uliosumbua sana chati za muziki “KUACHWA”.

“Kuachwa” ni wimbo uliotungwa na Khalid Chokoraa zaidi ya miaka mitano iliyopita, enzi hizo akiwa na Twanga Pepeta ambapo aliwashirikisha Jose Mara, Kalala Jr na Chaz Baba.

Hiyo ilikuwa ni kazi binafsi ya Chokoraa nje ya bendi, ikiwa ndani ya albam iliyopewa jina hilo hilo la ‘Kuachwa” huku ndani yake ikiwa na nyimbo nyingine kali zilizowashirikisha wasanii tofauti tofauti.

Kiroho safi kabisa, Twanga Pepeta ikiamini asilimia 80 ya waliotengeneza albam ya “Kuachwa” ni watoto wa nyumbani, imeandaa onyesho hilo la ‘Usiku wa Kuachwa” ili kuwapa mashabiki  uhondo wa vitu adimu.

Mmoja wa wakurugenzi wa Aset inayomiliki Twanga Pepeta, Omar Baraka ameiambia Saluti5 kuwa mbali ya nyimbo kali za albam ya “Kuachwa” pia zitapigwa nyimbo kali za Twanga Pepeta na Mapacha Watatu.
Kutoka kushoto ni Kalala Jr, Jose Mara, Chaz Baba na Khalid Chokoraa wakati wakithibitisha kushiriki onyesho la "Usiku wa Kuachwa" litakalofanyika Novemba 28 ndani ya Mango Garden Kinondoni

MANCHESTER UNITED BILA ROONEY WALA ANTHONY MARTIAL YAICHAPA WATFORD 2-1

$
0
0
Hakuna Wayne Rooney. Hakuna Anthony Martial lakini bado hakuna tatizo, Manchester United wanavuna pointi tatu muhimu.

Wakicheza ugenini dhidi ya Watford katika mchezo wa Premier League, United wanaibuka na ushindi wa bao 2-1, ushindi uliokuja kwa mbinde baada ya wenyeji kutawala sehemu kubwa ya mchezo.

Alikuwa ni Memphis Depay ndiye aliyeipatia United bao la kuongoza dakika ya 11 baada ya kuunganisha mpira uliotoka kwa Ander Herrera.

Troy Deeney aliizawazishia Watford kwa penalti ya dakika ya 87 lakini ni Deeney huyo huyo aliyeipa ushindi Manchester United baada ya kujifunga dakika ya 90 kufuatia krosi iliyopigwa kwenye kisanduku cha sita na Bastian Schweinsteiger.

WATFORD (4-4-2): Gomes 6, Nyom 5 (Paredes 69, 6), Cathcart 6, Britos 6, Anya 6, Capoue 7.5, Watson 5.5, Abdi 6.5, Deeney 7, Jurado 4.5 (Ake 45, 6), Ighalo 6.5

MANCHESTER UNITED (4-2-3-1): De Gea 6.5, Young 7, Jones 7.5 (McNair 69, 6), Smalling 7, Blind 6, Schneiderlin 8.5, Schweinsteiger 7.5, Mata 6.5 (Pereira 79, 6), Herrera 6.5 (Rojo 25, 5.5), Lingard 7, Depay 8
Bastian Schweinsteiger (right) wheels away in celebration after his cross was turned into his own net by Watford striker Troy Deeney
Bastian Schweinsteiger (kulia) akikimbia kushngalia baada ya kusababisha bao la ushindi la Manchester United 
Moments before, Deeney confidently stepped up and fired his spot-kick past David de Gea to level the scores at Vicarage Road
Muda mfupi baada ya Deeney kuisawazishia Watford kwa njia ya penalti 
Manchester United goalkeeper De Gea celebrates after his team scored a late second-half winner to defeat Watford 
Kipa Manchester United De Gea akishangilia baada ya timu yake kufunga bao la pili
Memphis Depay met Ander Herrera's superb delivery to open the scoring for Manchester United at Vicarage Road in the 11th minute
Memphis Depay akiunganisha mpira wa Ander Herrera kuifungia Manchester United bao la kuongoza
The Holland winger wheels away to celebrate his goal after shrugging off his marker to score his second Premier League goalDepay winga wa kimataifa wa Holland akifurahia bao lake ambalo ni la pili kwake katika Premier League 
Depay, who has endured a slow start to his United career after arriving from PSV in the summer, is mobbed by his team-mates
Manchester United wakimpongeza Depay


CHELSEA YAONA MWEZI, YAILAMBA NORWICH 1-0

$
0
0
Hatimaye Chelsea imeepukana na mwenendo mbovu Premier League baada ya kuilamba Norwich City 1-0.
Bao la dakika ya 64 kutoka kwa mshambuliaji Diego Costa, lilitosha kabisa kuipa Chelsea ushindi muhimu unaotarajiwa kufufua ari ya kikosi hicho cha Jose Mourinho.
Diego Costa (left) fires homes the winner as he helped Chelsea claim a much-needed three points at Stamford Bridge
Diego Costa (kushoto) akiachia mkwaju ulioipatia Chelsea bao dakika ya 64
The striker is congratulated by Willian and salutes the crowd following his fine individual goal
Diego Costa akipongezwa na Willian 
The Spaniard, goes for a loose ball inside the Canaries box but the away side cleared their lines
Diego Costa akiifungia Chelsea bao pekee

ARSENAL YASHIKWA PABAYA NA WEST BROM ...yashushwa hadi nafasi ya nne

$
0
0
Kwa mara nyingine tena, Arsenal imeshindwa kukaa juu ya mismamo wa Ligi Kuu pale iliporuhusu kipigo cha bao 2-1 kutoka kwa West Bromwich Albion.

Arsenal itabidi ijilaumu yenyewe kwa kushindwa kuambulia japo sare baada ya kiungo Santi Cazorla kukosa penalti dakika ya 84.

Ni Arsenal waliokuwa wa kwanza kupata goli dakika ya 28 kupitia kwa mshambuliaji Olivier Giroud aliyefunga kwa bao tamu la kichwa ambalo lilidumu kwa dakika nane tu kabla ya James Morrison kufunga kwa shuti kali dakika ya 35.

Dakika tano baadae Arsenal waliokuwa ugenini, wakaruhusu bao la pili lililokuja kwa njia ya kujifunga kupitia kwa kiungo Mikel Arteta. Kipigo hicho kimeiporomosha Arsenal hadi nafasi ya nne.

West Brom: Myhill 6.5; Dawson 7, Evans 7, Olsson 7.5, Brunt 7; Yacob 7, Fletcher 7; Sessegnon 6 (Gardner 61’ 5), Morrison 7 (Lambert 77’ 5), McClean 6.5; Rondon 6 (Berahino 68’ 6)

Arsenal: Cech 6; Bellerin 6, Mertesacker 6, Koscielny 6, Monreal 6; Coquelin 5 (Arteta 14’ 3 (Flamini 48’ 5), Cazorla 6; Sanchez 6, Ozil 6, Gibbs 5 (Campbell 63’ 4); Giroud 7
Santi Cazorla botches a late penalty effort that would have secured a share of the spoils for Arsenal with six minutes remaining Santi Cazorla akiteleza na kukosa penalti
West Brom take the lead at The Hawthorns as Mikel Arteta turns James McClean's cut-back into his own net five minutes before half-time West Brom wakipata bao la ushindi kupitia goli la kujifunga la Mikel Arteta dakika tano kabla ya mapumziko
Arsenal goalkeeper Petr Cech (right) exchanges a glance with his team-mate Arteta after his costly own-goal in the first-half Kipa wa Arsenal  Petr Cech (kulia) akimfariji Arteta baada ya kujifunga
McClean (left) and Salomon Rondon celebrate as Tony Pulis' side secure a precious lead approaching the half-time break 
McClean (kushoto) na Salomon Rondon wakishangilia bao la pili la West Brom
Cech cuts a frustrated figure on the pitch as the Gunners gave up two goals in the space of five minutes Cech akiwa hoi baada ya kufungwa bao la pili
The Gunners striker slides on the deck in front of the travelling Arsenal supporters following his effort just before the half hour mark 
Giroud akishangilia bao pekee la Arsenal

LIVERPOOL YAIPA KISAGO CHA MBWA MWIZI MANCHESTER CITY NA KUWASHA INDIKETA PREMIER LEAGUE

$
0
0
Manchester City wakiwa kwenye uwanja wao wa Etihad wamechukua kipigo kitakatifu kutoka kwa Liverpool katika mchezo mkali wa Premier League ulioshuhudia nyavu zikitikisika mara tano.

Hadi dakika ya 32 tayari Liverpool iliyoibuka na ushindi wa 4-1,  ilikuwa mbele 3-0 kwa mabao ya Eliaquim Mangala aliyejifunga dakika ya 8, Philippe Coutinho dakika ya 23 na Roberto Firmino dakika ya 32.

Sergio Aguero akicheza mchezo wake wa kwanza baada ya kuwa majeruhi kwa wiki sita, akaifungia Manchester City bao pekee dakika ya 44 na kufanya timu hizo ziende mapumziko matokeo yakiwa 3-1.

Beki wa kati wa Liverpool Martin Skrtel akahitimisha kwa bao la dakika ya 81 na kumfanya kocha Jurgen Klopp aanze kuamini kuwa sasa lolote linaweza kutokea katika mbio za kusaka taji la Premier League.
Adam Lallana is all smiles after Liverpool open the scoring at the Etihad Stadium thanks to an own goal by Eliaquim Mangala (centre)Adam Lallana (kulia) akifurahi baada beki wa City Eliaquim Mangala (katikati) kujifunga
Liverpool ace Philippe Coutinho (right) doubled the scoreline at Manchester City after linking up with his compatriot Roberto FirminoLiverpool ace Philippe Coutinho (right) doubled the scoreline at Manchester City after linking up with his compatriot Roberto Firmino
Firmino turned from provider to goalscorer as he put his side 3-0 up after just 32 minutes of the Premier League clash in Manchester
Firmino akishangilia baada ya kuifungia Liverpool bao la tatu
Man City striker Sergio Aguero scored a consolation goal on his return from injury but he could not help his side get back into the game
Mshambuliaji wa Man City Sergio Aguero akiifungia timu yake bao la kufutia machozi
Liverpool centre back Martin Skrtel slides on his knees in celebration of his side's fourth goal at Manchester City's home groundSentahafu wa Liverpool Martin Skrtel akishangilia bao lake




BARCELONA MOTO CHINI, YAIPIGA REAL MADRID 4-0 NDANI YA SANTIAGI BERNABEU

$
0
0
Santiago Bernabeu ilkuwa kimya wakati Barcelona ikiimiminia magoli Real Madrid pale mahasimu hao walipokutana kwenye mchezo wa El Classico ya La Liga.

Barcelona wakaibuka na ushindi mnono wa bao 4-0 huku Luis Suares akiwa mwiba kwa kufunga mara mbili katika dakika ya 11 na 74.

Neymar naye hakubaki nyuma, aliifungia Barcelona bao la pili dakika ya 39 huku Iniesta akitupia wavuni bao la tatu dakika ya 53.

Real Madrid XI: Navas, Danilo, Ramos, Varane, Marcelo (Carvajal - 55), Modric, Bale, Kroos, Rodriguez (Isco - 55), Ronaldo, Benzema

Barcelona XI: Bravo, Alba, Pique, Mascherano (Mathieu - 27), Alves, Busquets, Iniesta (Munir - 77), Rakitic (Messi - 57), Roberto, Suarez, Neymar
Luis Suarez (left) fires home the opener for Barcelona as they shocked arch-rivals Real Madrid at the Bernabeu Luis Suarez (kushoto) akiifungia Barcelona bao la kwanza 
The former Liverpool striker wheels away in celebration as the Catalonian side took control early on
Mshambuliaji wa zamani wa Liverpool akishangilia baada ya kufunga dakika ya 8
 Brazilian superstar Neymar celebrates after doubling the lead from Andres Iniesta's brilliant through ballNeymar akiruka juu kushangilia goli lake
The Spanish maestro then found the net himself with a thumping finish from the edge of the Real box
Iniesta akitupia bao la tatu
Cristiano Ronaldo throws his hand up in frustration after missing a golden opportunity to pull one backCristiano Ronaldo akijilaumu baada ya kukosa goli
Gareth Bale appeals for a foul after being brought down which summed up a disappointing night for Real Gareth Bale akimlalamikia mwamuzi
Barca's players walk over to the away fans at the end of the game as they thrashed their arch-rivalsWachezaji wa Barcelona wakishangilia baada ya mchezo kumalizika

ROMELU LUKAKU ANAKUWA MCHEZAJI WA TANO CHINI YA MIAKA 23 KUFUNGA MAGOLI 50 PREMIER LEGUE WAKATI EVERTON IKIIFUNGA ASTON VILLA 4-0

$
0
0
Mshambuliaji wa Everton Romelu Lukaku anakuwa mchezaji wa tano chini ya umri wa miaka 23 kufunga magoli 50 kwenye Premier League.

Lukaku amefikia hatua hiyo baada ya kufunga mara mbili katika mchezo dhidi ya Aston Villa kwenye uwanja wa Goodison Park ambapo Everton iliibuka na ushindi wa bao 4-0.

Lukaku ambaye atatimiza miaka 23 Mei 13, anaungana na Wayne Rooney, Cristiano Ronaldo, Robbie Fowler na Michael Owen kwenye orodha hiyo.

Mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Ubelgiji amefunga jumla ya magoli 51 akiwa na West Brom na Everton.
Romelu Lukaku celebrates after scoring his 50th goal in the Premier League on Saturday afternoon
Romelu Lukaku akisherehekea bao lake la 5o Jumamosi mchana
Lukaku achieved the milestone with a header to give Everton a 2-0 lead against Aston Villa on Saturday
Lukaku akiruka juu na kufunga kwa kichwa dhidi ya Aston Villa 
The 22-year-old scored his 51st goal in the Premier League soon after with a left-footed strikeLukaku  mwenye umri wa miaka 22 akifunga bao lake la 51 wakati Everton ilipomenyana na Aston Villa
Liverpool legend Robbie Fowler scored his 50th league goal at 20 years, eight months and eight days
Gwiji wa Liverpool Robbie Fowler alifunga bao lake la 50 Premier League akiwa na umri wa miaka 20 na miezi minane na siku nane 
Michael Owen scores against Leeds during a Premier League game early in his career at Anfield 
Michael Owen ni miongoni mwa makinda waliofunga mabao 5o wakiwa katika umri mdogo
Cristiano Ronaldo completes his hat-trick against Newcastle in Manchester United's 6-0 win January 2008
Cristiano Ronaldo akifunga hat-trick dhidi ya Newcastle wakati  Manchester United iliposhinda 6-0 Januari 2008
Manchester United striker Wayne Rooney celebrates after netting his 50th Premier League goal in 2006
Mshambuliaji wa Manchester United  Wayne Rooney akifunga bao lake la  50 la Premier League mwaka 2006

VAN GAAL AKIRI KUWANIA KUMSAJILI CRISTIANO RONALDO MSIMU UJAO

$
0
0
Kocha wa Manchester United  Louis van Gaal ameweka wazi kuwa atapambana kumsajili Cristiano Ronaldo iwapo mchezaji huyo ataamua kuondoka Real Madrid.

Ronaldo, 30, kwa muda mrefu amekuwa akihusishwa na kurejea Old Trafford hususan ndani ya miaka miwili iliyopita na sasa inaaminika kuwa ataruhusiwa kuondoka Bernabeu kiangazi kijacho huku kocha  Rafa Benitez akitarajiwa kuijenga timu kupitia Gareth Bale.

Mwaka 2o13 United ilijaribu kumsajili bila mafanikio mshindi huyo wa tuzo tatu za mchezaji bora wa dunia.

Lakini safari hii huku Louis van Gaal akilalamikia uhaba wa wachezaji wa pembeni kwenye kikosi chake, Mholanzi huyo amethibitisha kuwa Ronaldo yuko kwenye kikosi akili yake.

"Anacheza pembeni, ana kasi na anafunga magoli. Sidhani kama kuna kocha duniani ambaye asingependa kuwa nae," alisema kocha huyo wa Manchester United.

"Kwa hakika tunamfuatilia. Tunaangalia wachezaji wote, sio Ronaldo tu, lakini wachezaji wa aina hii ni ngumu kuwanasa. Wacha tusubiri na kuweka matumaini."
Bosi wa Manchester United Louis van Gaal ameweka wazi kuwa angependa kumsajili Cristiano Ronaldo msimu ujao
Ronaldo (left) looks set to leave the Santiago Bernabeu following the arrival of manager Rafa Benitez (right)
Ronaldo (kushoto) akiwa na Rafa Benitez 
Benitez has plans to build his Real Madrid side around Welsh star Gareth Bale (left), rather than Ronaldo
Benitez amedhamiria kuijenga Real Madrid kupitia kwa Gareth Bale (kushoto) kuliko Ronaldo

HIVI NDIVYO WANA NJENJE WALIVYOPAGAWISHA SALENDER BRIDGE DAR

$
0
0


MAMIA ya mashabiki wa mduara, juzi Jumamosi walipata raha ya aina yake pale bendi ya Kilimanjaro ‘Wana Njenje’ ilipomwaga burudani ya kufa mtu kwenye kiwanja chake cha nyumbani cha Salender Bridge, jijijni Dar es Salaam.
Saluti5 iliyotimba ukumbini hapo siku hiyo, ilishuhudia namna muziki mkali wa bendi hiyo ulivyokuwa ukiwacharusha mashabiki ambao wengiwao walishindwa kuvumilia kubaki vitini na kujikuta wakijimwaga katikati kucheza kila wimbo.
Licha ya bendi hiyo yenye mastaa wakongwe kama John Kitime, Waziri Ally na Nyota Waziri, kurindimisha vibao vyao vikali, lakini pia ‘damu changa’ nao waliipamba shoo hiyo kwa nyimbo za kukopi, hususan zile za Bongofleva.
Wana Njenje hutumbuiza kwenye ukumbi huo kila wiki katika siku kama hiyo ya Jumamosi, ambapo wapenda maraha wengi jijini Dar es Salaam hujitokeza kwa wingi na kufurahi.
Zifuatazo ni picha 10 za namna onyesho hilo lilivyonoga.

Kikosi kazi cha baadhi ya wanamuziki wa Njenje wakiwajibika jukwaani 


 Mwimbaji Abuu Mwinchumu akiwapagawisha mashabiki

Abuu Mwinchumu akiimba pamoja na Nyota Waziri

 Mkongwe John Kitime akicharaza kwa uhodari mkubwa gitaa la kati, Rythm huku mmoja wa mashabiki akimfuatilia kwa makini

'Mkaanga chips' Juma Omary akifanya vitu vyake

 Keppy Kiombile akicharaza gitaa la Besi
 Waziri Ally (kushoto), akiimba sambamba na Selemani moja ya vibao vya kukopi vya Bongofleva

 Mwimbaji Selemani aionyesha uwezo wake

 Nyota Waziri akiwachezesha mashabiki

 Waziri Ally akipapasa kinanda kwa mbwembwe

 John Kitime akipiga gitaa na kuimba twist

 Mwimbaji mahiri wa kopi za Bongofleva ambaye ni ndugu na Hemed Suleiman PHD, nae akifanya yake 

Hapa mwimbaji Selemani akiendelea kumwaga 'voko'

 Rhumba limekolea jukwaani

Waziri Ally na John Kitime wakiwasha moto

MONALISA CHINDA AANZA KUINADI MUVI YAKE MPYA YA "HOUSE OF MALIQ'S ALIYOIACHIA MWEZI SEPTEMBAYA

$
0
0


MWIGIZAJI mrembo wa Nollywood, Monalisa Chinda, ameanza kuinadi filamu yake mpya iitwayo ‘House of Maliq’s’.
Msanii huyo aiingiza sokoni filamu yake hiyo mpya Septemba, mwaka huu na sasa inaonekana kutesa.

STEVE NYERERE AKATAA KUWAPIGIA NDOGONDOGO WASANII WA BONGO MOVIE KWA RAIS MAGUFULI

$
0
0


ALIYEWAHI kuwa Mwenyekiti wa Bongo Movie, Steve Nyerere amesema ameulizwa kwa zaidi ya mara sita na rais John Magufuli kuhusu msaada wanaouhitaji, lakini ameshindwa kumjibu kutokana na wasanii wengi kutojitambua.
“Sikatai,” alisema Stive. “Nilishamwambia mheshimiwa rais, utapoteza pesa yako, niliwahi kumwambia mstaafu na hata huyu mpya pia, wasanii wengi wa Bongo hawajitambui.”
“Kwasababu ni lazima tukae chini tutafakari tunataka nini, mimi ni mtu niliyewahi kuulizwa na Magufuli zaidi ya mara sita, serikali haiwezi bila ya sisi wenyewe kujitambua, hata uweke mabilioni ya pesa,” alisisitiza.
Steve alisema wasanii wengi wamejivisha joho la usanii wa filamu lakini hawafanyi kazi na kwamba kuna zaidi ya asilimia 90 ya wasanii wa fani hiyo, ambao hawako makini na kwamba wamekuja tu kuuza sura.
Stive alisema kuwa, ni asilimia sita tu ama tano ya wasanii hao, ndio ambao wana nia ya kufanya kazi na wengine wameingia ili kupata majina na kufanya mambo yao mengine sio kuinua sanaa.
Alisema kuwa, kwa sasa sanaa ya filamu imefikia katika hali mbaya ambapo inaelekea kufa kabisa.

PAUL WA P. SQUARE AJIFICHA KUKIMBIA 'UGENI' SIKU YA BIRTH DAY YAKE

$
0
0


MSANII maarufu wa kundi la P. Square, Paul ambae ni pacha wa Peter Okoye, aliamua kujificha wiki iliyopita wakati wa kusheherekea siku yake ya kuzaliwa.
Habari zilizovuja zilisema, msanii huyo alijifungia kwake na kula keki ya ‘bd’ akiwa na watu wa familia yake tu.
Paul alisema siku moja baadae kwamba hakutaka kufanya sherehe ya kifahari na badala yake aliamini kuwa atafaidi sana akibaki na mkewe na mtoto wao.

BEN POL AUFAGILIA WIMBO WAKE WA “SOPHIA”

$
0
0


MKALI wa Hiphop hapa nchini, Ben Pol amesema kuwa wimbo wake wa Sophia umemfanya apate mashabiki wengi wapya, ambapo wengine wanadhani huo ndo wimbo wake wa kwanza.
Akiongea na Saluti5, Ben Pol alisema kuwa, wimbo huo umemfanya apate mialiko mingi hivi sasa kuliko ilivyokuwa hapo awali, huku akidai umempeleka mahali ambapo hakuwapo na hakutegemea kuwapo.
“Sophia imeniongezea mashabiki wapya wengi sana ambao hata walikuwa hawaijui kabisa, tena wanafikiri ndio wimbo wangu wa kwanza,” alisema Ben Pol.
Alisema kuwa, kwa mafanikio hayo pamoja na kupata mialiko mingi ya kufanya shoo, ni ishara kuwa wimbo huo umeeleweka, ambapo hivi sasa anajipanga kuachia kazi nyingine bora zaidi.

STAMINA AWASHUKURU MASHABIKI KWA WIMBO MPYA

$
0
0


MSANII tishio wa Hiphop, Bonaventure Kibogo ‘Stamina’, amewazawadia mashabiki wake wimbo ‘Bonus Track’, ikiwa ni kuwashukuru kwa kumfikisha alipo na kuwakumbusha historia yake ya muziki na maisha yake kabla na baada ya kutoka kwenye gemu.
Stamina ameachia wimbo huo unaokwenda kwa jina la ‘Mr. Bonaventure’ mwishoni mwa wiki, siku ambayo alikuwa akisherehekea kumbukumbu ya kuzaliwa na kusema kwamba anawashukuru mashabiki wake kupitia wimbo huo huku akiongeza kuwa wimbo rasmi utatoka hivi karibuni.
“Namshukuru Mungu, vyombo vya habari na mashabiki wangu, nimetanguliza huu wimbo kwao kama ‘bonus truck’ inayoelezea historia ya kazi yangu na maisha yangu, wimbo wangu official utatoka soon,” alisema Stamina.
Viewing all 8805 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>