Quantcast
Channel: saluti5
Viewing all 8805 articles
Browse latest View live

DOUBLE M SOUND SASA KUITWA DOUBLE M PLUS …Kupaza aisuka “Ganda la Mua” kivingine

$
0
0

Baada ya kusukwa upya bendi ya Double M Sound inayoongozwa Mwinjuma Muumin,  sasa itajulikana kama Double M Plus.

Mwinjuma Muumin amesema ameamua kukarabati jina la bendi yake ili kwenda sambamba na mabadiliko makubwa aliyoyafanya.

Muumin amedai Double M Plus itaibuka na nyimbo mpya zitakazoendana soko la sasa hivi ikiwa na wasanii wapya wenye uwezo wa hali ya juu.

Bendi hiyo imetambulisha wanamuziki wake wapya wakiwemo Dogo Rama, Saleh Kupaza na Jojoo Jumanne kutoka Twanga Pepeta.

Naye Saleh Kupaza amesema anashuka na wimbo mpya Double M Plus ambao utajulikana kama “Ganda la Mua”.

“Hii sio ile niliyotunga Twanga Pepeta, kwanza Twanga walilikataa lile jina, ninachojua mimi ni kwamba wimbo wangu ule hauna jina na umeachwa ukipotea kwa makusudi, kwahiyo “Ganda la Mua” inakuja kivingine ndani ya Double M Plus,” alisema Kupaza katika maongezi yake na Saluti5.


MASHAUZI CLASSIC KUZINDUA ALBAM YA “SURA SURAMBI” NOVEMBA 26

$
0
0

Kundi la Mashauzi Classic linatarajiwa kuzindua albam yake ya “Sura Surambi” Alhamisi ya Novemba 26 ndani ya ukumbi wa Mango Garden Kinondoni.

Meneja wa Mashauzi Classic, Ismail Sumaragar ameiambia Saluti5 kuwa nyimbo zote zinazounda albam hiyo zimekamilika.

Sumaragar amesema jumla ya nyimbo sita zinaunda albam ya “Sura Surambi” ambapo tatu ziliachiwa hewani miezi kadhaa iliyopita huku tatu nyingine zikiwa mpya kabisa.

Meneja huyo wa Mashauzi inayoongozwa na mwimbaji bora wa kike Isha Mashauzi,  amesema kutakuwa na burudani kadhaa za utangulizi.

ZUBEIDA MALICK WA MASHAUZI CLASSIC NAYE AKAMILISHA “MJINGA MPE CHEO” NDANI YA SOFIA RECORDS

$
0
0

Mwimbaji mwenye sauti tamu Zubeida Malick kutoka Mashauzi Classic Modern Taarab, amekamilisha wimbo wake mpya “Mjinga Mpe Cheo”.

Wiki hii Zubeida akiwa na kundi zima la Mashauzi, alijitosa ndani ya studio za Sofia Records chini ya producer Ababuu Mwana Zanzibar kurekodi wimbo huo utakaopatikana kwenye albam ya “Sura Surambi”.

Ngoma hiyo matata ni utunzi wake Isha Ramadhan “Queen of the Best Melodies” na imehitimisha kazi ya kurekodi nyimbo zote sita za albam hiyo ya “Sura Surambi” itakayozinduliwa Alhamisi ya Novemba 26 pale Mango Garden Kinondoni.

Ni wimbo wenye bonge la meseji huku ala zilizokung’utwa na Kalikiti Moto (kinanda), Rajab Kondo (bass) na Pishuu Meshaa (solo), zikikimbiza ile mbaya.
Zubeida Malick alipokuwa akirekodi wimbo mpya wa "Mjinga Mpe Cheo"

ENGLAND YAILAMBA UFARANSA 2-0 ...WAYNE ROONEY ANAHUSIKA

$
0
0
England imefuta machungu ya kipigo cha Hispania kwa kuitandika Ufaransa 2-0 katika mchezo kimataifa wa kirafiki uliopigwa kwe dimba la Wembley.

Bao la kwanza la England lilifungwa na kinda Dele Alli aliyekuwa akicheza mchezo wake wa kwanza kwa timu ya taifa huku goli la pili likifungwa na Wayne Rooney.

England beat France in their international match that was used to pay tribute to those who lost their lives in the Paris terror attacks
England imeifunga Ufaransa
Dele Alli marked his first start at international level with a stunning strike that gave England the lead at Wembley on Tuesday
Dele Alli alikuwa na siku njema baada ya kufunga kwenye mechi yake ya kwanza kwa timu ya taifa
Alli struck from long range to put England ahead against France in the first half of their match at Wembley in north London
Alli akiachia shuti kuiandikia England bao la kwanza
England captain Wayne Rooney volleyed home at the far post just after half-time to secure victory for the home side
Wayne Rooney akifunga bao la pili kwa England

ZLATAN IBRAHIMOVIC AIPELEKA SWEDEN EURO 2016

$
0
0
Zlatan Ibrahimovic ameifungia Sweden magoli mawili katika mchezo wa kufuzu Euro 2016 dhidi ya Denmark huku mechi hiyo ya vuta nikuvute ikimalizika kwa sare ya 2-2.

Sare hiyo inafanya Sweden ipate tiketi ya kwenda Euro 2016 kwa jumla bao 4-3 kufuatia ushindi wake wa 2-1 kwenye mchezo wa kwanza.

Denmark ikiwa nyumbani ililazimika kupambana baada ya kuwa nyuma kwa bao 2-0 lakini sare ya 2-2 bado haikuwasaidia kwenda kwenye fainali za Euro 2016.
Zlatan Ibrahimovic falls to his knees after the final whistle as Sweden celebrate reaching the Euro 2016 Finals
Zlatan Ibrahimovic akipiga magoti kushukuru Mungu
Ibrahimovic scores a second-half free-kick to make sure of Sweden's place at Euro 2016 next summer
Ibrahimovic anafunga kwa free-kick kipindi cha pili ba kuihakikishia Sweden tiketi ya  Euro 2016 kiangazi kijacho
The Paris Saint-Germain striker curled the ball home with his trademark panache as Denmark were beaten in the second leg
Mshambuliaji huyo wa Paris Saint-Germain akifunga bao maridadi
Ibrahimovic watches as the ball curls over the wall and into the top corner of the net to put daylight between Sweden and Denmark
Ibrahimovic akitazama mpira wake ukielekea wavuni




OMARY TEGGO, WANAWE KUTAMBULISHA NYIMBO ZAO EQUATOR GRILL DESEMBA 9

$
0
0


BENDI ya mipasho ya Coast Modern Taarab Desemba 9, mwaka huu itafanya uzinduzi wa albamu yake mpya inayokwenda kwa jina la ‘Mama Kijacho’, huku wasanii kibao wakiwa wamepangwa kunogesha.
Baadhi ya wasanii walioalikwa kunogesha shughuli hiyo ambayo kiingilio chake kitakuwa ni sh. 5,000, ni pamoja na ‘Malkia wa Mipasho’ Khadija Kopa, Isha Mashauzi ‘Queen of the Best Meodies’ na ‘Mfalme wa Vigodoro’ Msagasumu.
Akizungumza jijini Dar es Salaam jana, Yussuf Teggo alisema, mbali ya wasanii hao kunogesha, uzinduzi huo pia utapambwa na burudani ya utambulisho wa ujio wa ‘Vijukuu wa Teggo’ ambao ni Khairaty na Taliq Teggo.
Teggo alivitaja vibao vilivyomo kwenye albamu hiyo na waimbaji wake kwenye mabano kuwa ni chenyewe, ‘Mama Kijacho’ (Maua Teggo), ‘Nimempata Mrihti’ (Omar Teggo) na ‘Shari Si Kitu Kwangu’ (Aisha Masanja).
Kadhalika, Teggo anayefahamika pia kama ‘Anko Meneja’, aliema kuwa pia katika albamu hiyo, kuna wimbo uitwao ‘Hayo Yote ya Kukosa’ ambao umeimbwa na Omary Teggo kwa kushirikiana na Mwinyimkuu wa Le Grand Utalii.

UVAAJI WA NGUO FUPI KWA WASANII WA KIKE WAMKERA BLESSING EFFIOM EGBE

$
0
0


MTAYARISHAJI mwanamama wa filamu za Nollywood, Blessing Effiom Egbe, amewaonya wasanii wa kike kuacha kuvaa nguo fupi za mitego kwani zinawashawishi wanaume na baadae kujikuta wanaandamwa na wanaume wengi wasioweza kuwakwepa.
Alisema hakuna mwanaume anaeweza kuvumilia kuona msichana akiwa nusu uchi asisisimkwe na baada ya hapo mitego huanza na mwisho msichana kujikuta anatembea na wanaume wengi kabla ya kuolewa.
Msanii uyo alizidi akisema kwamba uzoefu unaonyesha mwanamke akitembea na wanaume wengi ni vigumu kuachana nao wote hata atakapoolewa.
Alisema, hilo ndilo linalosababisha ndoa za masupastaa wengi kuvunjika ndani ya muda mfupi, kwani badhi yao hawakubali kusahau yaliyopita japo wanajua umeolewa.

YAMOTO BAND WAMTOA KIMASOMASO ZENA MOHAMMED WA OGOPA KOPAZ

$
0
0



VIJANA wanaotikisa katika muziki wa dansi la kizazi kipya, Yamoto Band, wamemtoa kimasomaso mwanamipasho Zena Mohammed, kwa kumpa shavu kwenye kibao chao kipya kinachokwenda kwa jina la ‘Mama’.
Bosi wa Yamoto Band na Diwani wa Kata ya Kilungule, Said Fella alisema, wameamua umshirikisha Zena kwenye wimbo huo ili kuwaonyesha mashabiki kuwa mwanadada huyo bado wamo kwenye gemu.
Fella alisema kuwa, kama lilivyo jina la wimbo, Zena amesimama kama mama, ambapo vijana wa Yamoto Band wanawawakilisha wanajamii wengine wote katika kumpongeza kwa kuzaa na kulea.
“Wimbo huo ambao kama ilivyo kwa vibao vetu vingine, nao tunaamini utawashika mashabiki wengi wa rika mbalimbali, tutauachia Desemba 15, mwaka huu,” alisema Fella.

TOKE MAKINWA AMBEMBELEZA MTALAKA WAKE ‘KULA MATAPISHI’

$
0
0


MWIGIZAJI mahiri wa Nollywood, Toke Makinwa licha ya kutamba wakati akiachana na mumewe Maje Ayida, amejirudi na sasa anaomba warudiane.
Habari kutoka kwa watu wa karibu wa mastaa hao zinasema Toke ameshamtumia watu kadhaa Maje kutaka suluhu akisema amemsamehe anaomba naye amsamehe na warudiane.

ANTHONY MARTIAL WA MANCHESTER UNITED ATEMBELEA MAGONGO, AUMIA KATIKA MECHI YA ENGLAND NA UFARANSA

$
0
0

Manchester United inapita katika kipindi kufuatia kuumia kwa mashambuliaji wake tegemeo Anthony Martial.

Mshambuliaji huyo wa kimatafa wa Ufaransa aliumia wakati akiitumikia nchi yake kwenye mchezo kimataifa wa kirafiki dhidi ya Ufaransa kwenye uwanja wa Wembley Jumanne usiku.

Katika mchezo huo ambao England ilishinda 2-0, Anthony Martial alitolewa dakika ya 67 ambapo baadae mguu wake ulifungwa bandeji huku akitembelea magongo.
Manchester United team-mates Wayne Rooney and Martial embrace on the Wembley pitch during the game
Wayne Rooney  na akmfariji Martial 
Martial makes his way off the field to be replaced by Atletico Madrid star Antoine Griezmann on 67 minutes
Martial akitoka na kumpisha nyota wa Atletico Madrid Antoine Griezmann dakika ya 67

HATIMAYE ARSENAL YAAMUA KUMALIZANA NA ALEXIS SANCHEZ

$
0
0
Arsenal inakaribia kumalizana na mshambuliaji wake Alexis Sanchez juu ya mkataba mpya utakaomweka Emirates kwa miaka mitano zaidi.

Inaaminika nyota huyo wa kimataifa wa Chile tayari ameshakubali ofa ya mkataba mpya wa miaka mitano kwa mshahara wa pauni 155,000 kwa wiki.

Sanchez amebakiza miaka miwili na nusu kwenye mkataba wake wa sasa hivi unaomwingizia pauni 130,000 kwa wiki. 

Arsenal inataka kuhakikisha mkali huyo haingii kwenye miaka yake miwili ya mwisho kabla hajasaini mkataba mpya.
Arsenal's Alexis Sanchez, pictured during international duty on Monday, is close to securing a new deal
Alexis Sanchez yuko mbioni kusaini mkataba mpya Arsenal
Star man Sanchez is close to agreeing a new five-year deal worth £155,000-a-week with the GunnersSanchez anakaribia kusaini dili la  £155,000 kwa wiki
Discussions with the forward are at an advanced stage and Arsenal believe a deal has been agreed
Inaaminika mazungumzo ya dili jipya la Sanchez ndani Arsenal yamefika mahala pazuri


SERGIO AGUERO AIPANIA MECHI YA LIVERPOOL JUMAMOSI HII

$
0
0
Aguero shakes hands with Man City manager Manuel Pellegrini after coming off injured against Newcastle
Mshambuliaji wa Manchester City Sergio Aguero amesema anafanya kila awezalo ili awe fiti kwa mchezo wa  Premier League Jumamosi hii dhidi ya Liverpool.

Aguero amekuwa nje ya dimba kwa wiki sita kufuatia maumivu ya msuli aliyoyapata Oktoba 9 wakati alipokuwa akiitumikia timu yake ya taifa ya Argentina dhidi ya Ecuador.

Mshambuliaji huyo bingwa wa kuzifumania nyavu hakuichezea Manchester City tangu ilipomenyana na Newcastle ambapo yeye mwenyewe alisukumiza wavuni mabao matano ndani ya dakika 20.

Aguero ameanza mazoezi kamili wiki hii na anaonekana kupania kushiriki mpambano wa Jumamosi kwenye dimba la Etihad Stadium.

"Natumai nitaweza kucheza mchezo huu," Aguero ameiambia tovuti ya klabu (www.mcfc.co.uk). "Ninafanya kila niwezalo kwa nguvu zangu zote kuwa fiti kwa mchezo wa Jumamosi."
Sergio Aguero celebrates scoring one of five goals he netted against Newcastle at the beginning of October
Sergio Aguero akishangilia moja ya mabao yake



KASHFA YA MAPENZI NA MBWA YAMTIKISA COSSY ORIJIAKOR

$
0
0


MWIGIZAJI asiyejali wa Nollywood, Cossy Orjiakor, alijifanya kutojali zaidi pale alipoibuka na kashfa nzito kwamba amefanya mapenzi na mbwa.
Hata hivyo, mrembo huyo ambaye pia anadaiwa kuishi na virusi vya ukimwi, amekurupuka na kusema, wanaompakazia wanamuonea wivu.  
Cossy hivi sasa anapata wakati mgumu kuinadi filamu yake mpya na sasa anajutia kuchelewa kukanusha kashfa ya kufanya mapenzi na mbwa ambaye marafiki zake walidai kuwa alifanya hivyo kwa kutafuta ujiko.

CHRISTINA MILIAN AMWAGA MACHOZI RUNINGANI KULILIA PENZI LA LIL’ WAYNE

$
0
0


RAPA machachari Lil’ Wayne amemliza machozi aliyekuwa mpenzi wake, Christine Flores maarufu kama ‘Christina Milian.’
Christina ambaye ni mwanamuziki, mtunzi na mwigizaji, alimwaga machozi mbele ya televisheni ya taifa baada ya kukumbukia alivyoumizwa na Lil’ Wayne.
Mrembo huyo alisema mapenzi yao yalikuwa ya siri na hakuna aliyejua hadi walipoachana baada ya kumfumania rapa huyo akiwa na mwanamke mwingine nyumbani kwake.
“Lil’ Wayne ni muuaji, mwanaume asiejali utu, ni mnyama asie kifani, sasa nimejua ni kwa nini mkewe Toya Wright aliamua ndoa yao ivunjike,” alisema Christina huku akimwaga machozi.

BI MWENDA SASA ADAI YEYE KUITWA MCHAWI NI MAFANIKIO MAKUBWA

$
0
0


MKONGWE wa kike wa sanaa ya muvi, Fatma Makongoro ‘Bi Mwenda’, amebainisha kwamba tofauti na ilivyokuwa awali, hivi sasa anafurahia anakabiliwa na mtu na kuambiwa kinagaubaga kuwa ni mchawi, kutokana na mara nyingi kuonekana akiigiza hivyo.
Akiongea na Saluti5 Bi Mwenda alisema kuwa, hasira na machungu yote aiyokuwa nayo kipindi cha nyuma vyote vimemalizika kwa sasa, kutokana na kuamini kuwa kuitwa mchawi ni sehemu ya mafanikio yake katika tasinia ya filamu.
“Nimegundua kuwa, hadi kufikia mashabiki wangu kunikimbilia njiani ninapopita mitaani na kuniita jina la mchawi ni ishara kwamba, ujumbe ninaoutoa unaifikia hadhira kwa nguvu na kasi kubwa,” alisema Bi Mwenda.
Bi Mwenda aliyeanza kujipatia umaarufu mwanzoni mwa miaka ya 2000, alipokuwa katika kundi la Kaole sanaa Group, amekuwa akisifika kutokana kuuva kwake vizuri uhusika wa kichawi anaopendelea kuigiza kwenye filamu tofauti.

DAVIDO AONYESHA JEURI YA FEDHA NIGERIA

$
0
0


MSANII wa Hiphop anayetikisa kwa sasa nchini Nigeria, David Adedeji Adeleke marufu kwa jina la ‘Davido’, ameonyesha jeuri ya fedha.
Msanii huyo aliyeingia katika muziki mwaka 2011, amepiga hatua kubwa kimaendeleo na majuzi amekamilisha kujenga jumba la kifahari katika viunga vya jiji la Lagos.
Davido mwenye miaka 23, ametupia picha kwenye mtandao wake wa kijamii wa twitter unaoonyesha magari matatu ya kifahari yakiwa kwenye jumba hilo na kusema anatarajia kuhamia hivi karibuni.

TUPIA MACHO VIDEO YA “NIKUPETIPETI” (MAHABA NIUE) KUTOKA KWA AMIRY AKIMSHIRIKISHA ASLAY

$
0
0
Hii ni ngoma iliyotoka kitambo kidogo kwa njia ya audi huku mashabiki wengi wakiamini ni wimbo wa Yamoto Band.

“Nikupetipeti” inayofahamika zaidi kama “Mahaba Niue” ndio wimbo unaozungumziwa hapa, ikiwa ni kazi yake Amiry akimshirikisha Aslay kutoka Yamoto Band.

Ni audio iliyotengenezwa kwa hisani kubwa ya taasisi ya Mkubwa na Wanawe inayoongozwa na Said Fella.

Hata hivyo Amiry sasa ameamua kuachia video ya ngoma hiyo kali, lakini safari hii anaifanya kazi hii akiwa kivyake vyake nje ya mwamvuli wa Mkubwa na Wanawe.

Ni video iliyosubiriwa kwa hamu kubwa sana na mashabiki wa muziki. Itupie macho hapo juu.

ANDREY COUTINHO HABANDUKI YANGA

$
0
0

KIUNGO mshambuliaji wa Yanga, raia wa Brazil, Andrey Coutinho, alikuwa katika mchakato wa kukipiga barani Asia, lakini sasa atabaki Yanga, imefahamika.

Kwa mujibu wa habari za uhakika ambazo Saluti5 imezipata, Coutinho ambae hivi sasa yuko kwao Brazil kwa matatizo ya kifamilia, anatarajia kurejea nchini Jumamosi hii.

Mchezaji huyo aliyepata kuichezea klabu ya Rhukapura United ya Ligi Kuu Myanmar, aliwasiliana na klabu kadhaa za mataifa kadhaa ya Asia lakini wakala aliyekuwa akimuunganisha amesema dili imeshindikana ingawa hajafafanua.

Kutokana na maamuzi hayo, mchezaji huyo anapaswa kupigania namba kwenye kikosi cha Yanga ili kujitengenezea soko katika usajili ujao.

Imeelezwa kuwa Yanga ilikuwa ikivizia kumuuza mchezaji huyo na ingejaza nafasi yake kwa kusajili mchezaji wa kigeni.


Kutokana na kukwama huko, kocha Hans Van Der Pluijm atalazimika kufuta mpango wa kuongeza mchezaji wa kigeni kwa sasa.

TFF YATANGAZA TENDA KUWEZESHA TIKETI ZA ELEKTRIONIKI

$
0
0

KATIKA kile inachoonekana na kuteswa na jinamizi la kufeli kwa tiketi za elektroniki, Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), limetangaza tenda.

TFF kwa kushirikiana na mzabuni wa tenda hiyo ya elektroniki, benki ya CRDB, wametangaza tenda ya kusaka mshauri wa mfumo wa elektroniki.

Jukumu la mshauri huyo ni kupitia na kuwashauri namna ya kuondoa mapungufu yaliyopo katika mfumo wa uuzaji tiketi wa elektroniki katika michezo ya igi Kuu ya Vodacom Tanzania.

TFF imetangaza tenda hiyo, ili kumpata mshauri wa mfumo huo wa tiketi za elektroniki ambao ulisimamishwa na serikali Aprili, mwaka huu.

Kusimamishwa kwa matumizi ya tiketi za elektroniki kulitokana na kupungua kwa mapato tofauti na ilivyotarajiwa pamoja na kusababisha usumbufu mkubwa, ikiwamo mashine kugoma wakati mashabiki wameshanunua tiketi jambo lililosababisha mara kadha kutokea vurugu.

Katika tarifa yake, TFF imesema maombi ya tenda yawasilishwe katika ofisi ya katibu Mkuu wa TFF iliyopo uwanja wa Karume, jijini Dar es Salaam, kuanzia saa 3:00 asubuhi hadi sa 10:00 jioni, siku za kazi, Jumatatu hadi Ijumaa.

Gharama ya fomu ya kuombea tenda hiyo ni sh. 100,000 na mwisho wa kuwasilisha maombi ni Desemba 17, mwaka huu.

UTEMI WAMPONZA ERYKAH BADU KUZAA NA MIDUME MITATU TOFAUTI

$
0
0


MSANII Erykah Badu amejikuta akiponzwa na utemi wake uliomsababishia kuzaa na wanaume watatu tofauti.
Sababu ya kuzaa na wanaume hao ni utemi aliokuwa nao Erykah Badu ambaye huona fahari kuwachukua kitemi wanaume hao mbele ya wapenzi wao wa kike na kuondoka nao.
Mmoja wa marapa aliozaa nao amefichua kuwa Erykah alimchukua mbele ya mpenzi wake kwa kumkwida na kumwambia; “Leo twende nikakupe vitu adimu achana na huyo…”
Viewing all 8805 articles
Browse latest View live


<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>