Hatimaye kipa Gianluigi Buffon wa Juventus amefungwa na Lionel Messi kwa mara ya kwanza wakati miamba hiyo ya Italia ikisalimu amri mbele Barcelona kwa kufungwa 3-0.
Katika mchezo huo wa kundi D wa Ligi ya Mabingwa, Messi ambaye hapo kabla hakuwahi kumfunga Buffon hata mara moja, akatupia wavuni mabao mawili. Goli lingine la Barcelona lilifungwa na Ivan Rakitic.
Barcelona: Ter Stegen; Semedo, Pique, Umtiti, Alba, Busquets, Rakitic (Paulinho 77), Iniesta (Andre Gomes 83); Dembele (Sergi Roberto 81), Messi, Suarez.
Wafungaji: Messi 45, 69, Rakitic 56
Juventus: Buffon, De Sciglio (Sturaro 41), Benatia, Barzagli, Sandro, Pjanic, Matuidi, Bentancur (Bernardeschi 63), Dybala, Douglas Costa, Higuain (Caligara 87).
Na katika mechi ngingine ya kundi D, Olympiacos ikiwa nyumbani ikachpwa 3-2 na Sporting.