BEKI mpya wa Yanga, Fiston Kayembe ameanza kazi ya kujifua na kikosi hicho lakini haraka akatema cheche akisema atakaop saini mkataba jangwani ana uhakika atakuwa kikwazo cha washambuliaji nyota wa ligi kuu.
Faston amesema kwa sasa anataka kufanya kitu kuweza kumshawishi kocha wake George Lwandamina na kwamba hana wasiwasi katika kupewa mkataba na klabu hiyo lakini mara atakapomalizana na uongozi wa klabu hiyo na kuja kuanza kazi Novemba 15 anataka kuja kuipa makali safu ya ulinzi ya Yanga.