Quantcast
Channel: saluti5
Viewing all 8805 articles
Browse latest View live

DE GEA KUAONDOKA MANCHESTER UNITED IWAPO VAN GAAL HATATIMULIWA

$
0
0
Kipa wa MANCHESTER UNITED  David de Gea huenda akaandoka Old Trafford kiangazi hiki iwapo Louis van Gaal ataendelea kuwa kocha wa klabu hiyo msimu ujao.
Van Gaal bado ana mwaka mmoja kwenye mkataba wake na kuna matarajio madogo kuwa atapewa nafasi ya kumaliza mkataba huo.
Ingawa Van Gaal anaamini kuwa De Gea yuko na furaha Old Trafford, lakini watu wa karibu na mlinda mlango huyo wanabainisha kuwa kuendelea kuwepo kwa Van Gaal kutafungua milango wa De Gea kutimka Manchester United.
Inaelezwa kuwa De Gea, kipa wa kimataifa wa Hispania mwenye umri wa miaka 25, haamini katika mfumo wa Van Gaal.



MANCHESTER UNITED YAMALIZIA KIPORO CHAKE KWA USHINDI ...RASHFORD ATAKATA, ROONEY AFUNGA BAO LA 100 OLD TRAFFORD

$
0
0
The former England international winger is congratulated by team-mates after coming on to score United's third
Manchester United imeichapa AFC Bournemouth 3-1 katika wa mwisho wa Ligi Kuu ya England uliochezwa Old Trafford Jumanne usiku.

Matokeo ya mchezo huo ambao uliopaswa kufanyika Jumapili na kuahirishwa baada ya tishio la kuwepo bomu kwenye uwanja huo, hayajabadili chochote katika mbio za kusaka tiketi ya Ligi ya Mabingwa msimu ujao.

Wayne Rooney aliifungia United bao la kwanza dakika ya 43 akimalizia kazi nzuri ya Anthony Martial. Hilo linakuwa ni bao la 100 la Premier League kwa nahodha huyo wa England na Manchester United katika uwanja huo wa Old Trafford.

Akicheza mchezo wa kwanza tangu aitwe timu ya taifa ya England, kinda Marcus Rashford akaifungia United goli la pili kunako dakika ya 75 kabla ya Ashley Young hajafunga goli la tatu ilipotimu dakika ya 87.

United imemaliza katika nafasi ya tano na sasa itacheza michuano ya Europa League msimu ujao.

MANCHESTER UTD (4-1-4-1): De Gea 6; Valencia 7, Smalling 6.5, Blind 6, Borthwick-Jackson 6.5; Carrick 7; Lingard 6, Mata 6 (Herrera 75'), Rooney 7.5, Martial 6.5 (Young 83'); Rashford 7 (Depay 78').

BOURNEMOUTH (4-4-2): Federici 6.5; Francis 6.5, Elphick 6, Cook 6, Daniels 7; Ritchie 6, Gosling 6, Surman 5.5, Pugh 7 (Gradel 66, 6); King 6.5 (Afobe 66, 6), Wilson 6.5 (Grabban 79).
Manchester United captain Wayne Rooney celebrates after scoring the opener with his 100th Premier League goal at Old Trafford
Wayne Rooney akishangilia bao lake la 100 kwenye uwanja wa Old Trafford katika Premier League 
The England international converted a superb cross by Anthony Martial to break the deadlock on 43 minutes
Nahodha wa England akiifungia United bao la kwanza dakika ya 43 kufuatia pasi ya Anthony Martial 
Marcus Rashford (centre), playing his first game since making England's preliminary Euro 2016 squad, celebrates scoring United's second
Marcus Rashford (katikati), aliyecheza mchezo wake wa kwanza Manchester United tangu alipochaguliwa kwenye kikosi cha England kwaajili ya Euro 2016, akishangilia bao lake
Substitute Ashley Young (centre) came on to score United's third goal from a beautifully lofted Rooney pass in the dying minutes
Winga aliyetokea benchi Ashley Young (katikati) akifunga kwa kuunganisha krosi tamu ya Rooney 
Hivi ndiyo Msimamo wa ligi ulivyo


MIKEL ARTETA 'AKIRI' YU NJIANI KUELEKEA MANCHESTER CITY

$
0
0
Manchester City iko mbioni kushinda vita vya kuwania saini ya kiungo mkongwe wa Arsenal anayeelekea kutundika daluga.

City inataka kumnasa nyota huyo wa Hispania mwenye umri wa miaka 34 ili akawe kocha msaidizi wa Pep Guardiola.

Mara baada ya mchezo wa mwisho wa Ligi Kuu baina ya Arsenal na Aston Villa, Arteta aliweka wazi kuwa ana ofa tatu mkononi za benchi la ufundi ikiwemo ya kwenda Machester City.
Mikel Arteta (centre) pictured looking upset as he leaves the pitch at the Emirates on Sunday
Mikel Arteta (katikati) akilia baada ya mchezo wake wa mwisho kwa Arsenal Jumapili iliyopita 
The 34-year-old Arsenal midfielder wants to find his first coaching role after retiring from playing football
Mikel Arteta akifarijiwa na wachezaji wenzake

Ofa zingine za ukocha usaidizi ambazo Arteta hakutaka kuzitaja zinahusishwa na Arsenal na Tottenham, lakini inaaminika kuwa  tayari City imepiga hatua kubwa mbele katika dili hilo.


TWANGA WANA JAMBO LAO MEI 28, FUNGA KAZI NI JUNI 4 …Ni Chokoraa au Chaz Baba?

$
0
0

Bendi ya The African Stars “Twanga Pepeta” kwa mara ya kwanza katika historia yao, watatambulisha albam yao mpya jijini Mwanza Jumamosi Mei 28.

Hiyo inakuwa ni albam ya 13 ya Twanga Pepeta ambapo albam zao 12 za mwanzo zote zilitambulishwa jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi wa Aset inayomiliki Twanga Pepeta, mamaa Asha Baraka, ameiambia Saluti5 kuwa onyesho hilo litafanyika ndani ya ukumbi wa Villa Park.

Katika onyesho hilo, Twanga Pepeta watasindikizwa na wenyeji wao Super Kamanyola Band.

Kuna uwezekano mkubwa wa kuwepo kwa ‘surprise’ ya ujio wa mwimbaji wa zamani wa Twanga ambaye huenda akatambulishwa katika onyesho hilo.

Duru za burudani zilizotua Saluti5 zinaweka wazi kuwa Twanga Pepeta imekamilisha dili la kumrejesha nyumbani mwimbaji mmoja kati ya Chaz Baba na Khalid Chokoraa.

Ingawa Chokoraa na Chaz Baba wote wamekanusha kuhusishwa na mpango huo, lakini habari za ndani zinasema kuna onyesho kubwa linaadaliwa Mango Garden Juni 4 kwaajili ya utambulisho rasmi wa mmoja wa waimbaji hao.

Asha Baraka alikataa kata kata kuwepo kwa nyendo hizo za kuwarejesha waimbaji hao, lakini mtu mmoja wa karibu na Aset ameiambia Saluti5 hakuna ubishi kuwa Chokoraa au Chaz Baba mmoja wao anarejea Twanga Pepeta na kwamba kitendawili hicho kitafumbuliwa Juni 4 Mango Garden.

JOHN TERRY ASAINI MKATABA MPYA WA MWAKA MMOJA CHELSEA

$
0
0
Terry will add to his 703 appearances for his boyhood club after agreeing new terms with Chelsea this week
Hatimaye John Terry amesaini mkataba mpya Chelsea utakaomwezesha kukipiga Stamford Bridge kwa mwaka mmoja zaidi.

Terry ambaye alikuwa njiani kutundika daluga, sasa atakuwa nafasi ya kuongeza idadi ya michezo 703 aliyoichezea Chelsea aliyojiunga nayo miaka 22 iliyopita.

Habari hizi zinaondoka kabisa ukungu uliotanda juu ya hatma ya nahodha huyo mwenye umri wa miaka 35 ambaye alionekana kama anataka kutupiwa virago vyake.

Mwezi Januari Terry alifichua kuwa klabu  haikuwa na nia yoyote ya kurefusha mkataba wake, hali iliyoonyesha kuwa ndoa ya beki huyo na Chelsea inaelekea ukingoni.
Chelsea captain John Terry has signed a new one-year contract with the Stamford Bridge club
Nahodha wa Chelsea John Terry ameongezewa mwaka mmoja wa kubakia Stamford Bridge

WAYNE ROONEY AUPA MKONO WA KWAHERI USHAMBULIAJI

$
0
0
Manchester United captain Wayne Rooney looks to the sky after scoring his 100th goal at Old Trafford
Mshambuliaji na nahodha wa Manchester United na Englanda Wayne Rooney amesema anafikiria kuhamishia soka lake kwenye nafasi ya kiungo.
Rooney ameyasema hayo baada kucheza vyema katika safu hiyo dhidi ya Bournemouth katika uwanja wa Old Trafford kwenye mchezo wa mwisho wa Ligi Kuu ya England.
Katika mechi hiyo ya Manchester United ilipata ushindi wa maba0 3-1, matokeo yaliwapa tiketi ya kucheza Europa League.
Rooney alifunga bao la kwanza kabla ya kumtengea pasi nzuri Ashley Young aliyefunga goli la tatu.
“Wakati mwingine unashawishika kubadili mazingira ya kazi yako na kwa sasa ni mimi ni bora zaidi kwenye eneo la kiungo,” alisema Rooney.

GRANIT XHAKA APALILIA NJIA YA KUJIUNGA NA ARSENAL

$
0
0
Borussia Monchengladbach midfielder Granit Xhaka is a £35million target for Arsenal
Uwezekano wa Granit Xhaka kutua Arsenal umeongezeka baada ya kiungo huyo wa Borussia Monchengladbach kukiri kuwa kucheza Premier League ni njozi yake ya tangu utotoni. 

Arsenal inadaiwa imepiga hatua kubwa kwenye maongezi ya kupata saini ya nyota huyo mwenye umri wa miaka 23 anayetajwa kuwa na thamani ya zaidi ya pauni milioni 35.

Duru za michezo zinasema tayari kiungo huyo ameshamalizana na Arsenal juu ya maslahi yake binafsi na huenda dili lake la uhamisho likakamilika kabla ya Euro 2016.

Nyota huyo wa kimataifa wa Switzerland ameiambia luninga ya SRF ya Switzerland: "Premier League sio lengo langu kuu, lakini ni njozi yangu ya tangu utotoni. Ni njozi inayoweza kukamilika."

The Switzerland international (right) admits a move to the Premier League would fulfil a 'childhood dream'
Borussia Monchengladbach (kulia) yuko mbioni kutua Arsenal 

LIVERPOOL SAWA NA NGOMA YA KITOTO …YAPIGWA 3-1 NA SEVILLA, KOMBE LAENDA HISPANIA

$
0
0

Liverpool keeper Simon Mignolet flails as Gamiero meets an excellent cross from Mariano to net from close range
Njozi za kocha Jurgen Klopp kutwaa taji la Ulaya katika msimu wake wa kwanza Liverpool, zimeota mbawa baada ya timu hiyo kulambwa 3-1 na Sevilla katika fainali ya Europa League.

Liverpool ilikuwa ya kwanza kupata bao kunako dakika ya 35 kupitia kwa Daniel Sturridge, lakini Sevilla wakachomoa dakika ya 46 kwa bao la  Kevin Gameiro.

Coke akaifungia Sevilla mabao mawili ya haraka haraka dakika ya 64 na 70 yaliyotosha kuimaliza Liverpool.

Fainali hiyo ilipigwa kwenye uwanja wa St. Jakob Park huko Basle, Switzerlandna hiyo inakuwa ni mara ya tatu kwa Sevilla ya Hispania kutwaa taji hilo.
The England international celebrates scoring opener with with his now customary dance moves
Daniel Sturridge akishangilia bao pekee la Liverpool

VIJANA JAZZ WAINGIA STUDIO KUMWIMBIA MAGUFULI

$
0
0

Bendi ya Vijana Jazz “Air Pambamoto” wiki hii itaingia studio kurekodi nyimbo mpya.

Wakiongea katika ofisi za Saluti5 Jumatano mchana, viongozi wa bendi hiyo Abadallah Mgonahizilu na Saburi Athumani walisema miongoni mwa nyimbo hizo mpya ni pamoja na mmoja utakaokuwa maalum kwaajili ya kumpongeza Rais Pombe John Magufuli kwa namna anavyoongoza kwa mafanikio serikali ya awamu ya tano.

Viongozi hao ambao pia ni waimbaji tegemeo wa Vijana Jazz wakaweka wazi kuwa bendi yao inajipanga upya baada ya kimya cha miezi kadhaa bila ya kuwa na maonyesho ya kudumu.
Waimbaji wa Vijana Jazz Abadallah Mgonahizilu (kushoto) na Saburi Athumani katika ofisi za Saluti5 Jumatano mchana

MICHAEL CARRICK KUONDOKA MANCHESTER UNITED ...ARSENAL YATAJWA KUMVIZIA

$
0
0
The 34-year-old was accompanied by his children, Jacey and Louise, for the victory over Bournemouth
Michael Carrick anaamini Jumanne usiku katika uwanja wa Old Trafford, alicheza mchezo wake wa mwisho kwa Manchester United kwenye uwanja wao wa nyumbani.

Kiungo huyo mwenye umri wa miaka 34 alisindikizwa na watoto wake, Jacey na Louise, wakati alipoiongoza United kuingia uwanjani kwenye mchezo wao wa mwisho wa Premier League msimu huu dhidi ya Bournemouth. 

Rio Ferdinand na Patrice Evra nao pia walisindikizwa na watoto wao katika mchezo wa mwisho Old Trafford, ishara inayoonyesha kuwa Carrick naye anaweza akatimka United baada ya fainali ya FA dhidi ya Crystal Palace Jumamosi huu.

United bado haijaonyesha nia ya kumbakiza Carrick kwa kile kinachoaminika kuwa inataka kuwekeza kwa vijana zaidi. Arsenal na Newcastle zinatajwa kuwania saini ya kiungo huyo iwapo ataachwa na Manchester United.
Midfielder Michael Carrick believes he has played his final game for Manchester United at Old Trafford
Kiungo Michael Carrick anaamini mwisho wake Manchester United  umewadia
Carrick is United's second longest-serving player after Wayne Rooney but hasn't been offered a new contract
Carrick (kushoto) na Wayne Rooney ndiyo watumishi wa muda mrefu waliosalia kwenye kikosi cha United

NEWS:NDEGE NYINGINE POTELEA ANGANI MISRI HABARI IKO HAPA ( SOMA ZAIDI)

$
0
0
Shirika moja la ndege la misri limetangaza tangazo kwa nchi hiyo kuhusu upotevu wa ndege aira ya (AIRBUSA320) Ndege hiyo iliyokuwa inatokea mjimkuu wa ufaransa Paris UFARANSA
taarifa kutoka katika vyumba vya mawasiliano ya uwanjani hapo vina sema "Ndege hiyo ilitoweka kuwenye mitambo ya rada mara baada ya kutoka uwanja wa ndege wa paris Maafisa wanaosimamia Safari za ndege uwanjani hapa wamesema ndege hiyo iliyokuwa na Abiri 59 na Wahudumu 10 Shirika hilo limesema kuwa ndege hiyo ilitoweka katika maeneo ya mashariki ya bahari ya Mediterranean, kilomita 16 ndani ya anga ya Misri.

KWA HABARI ZA UHAKIKA ENDELEA KUTEMBELEA (SALUTI5) BURUDANI ZAIDI

 

ARSENAL, MANCHESTER UNITED, MANCHESTER CITY KATIKA VITA YA KUWANIA SAINI YA JAMES RODRIGUEZ

$
0
0


KLABU za Arsenal, Manchester United na Manchester City, zinafuatilia kwa ukaribu hali inayoendelea kwa mshambuliaji James Rodriguez kuelekea uhamisho wa dirisha la kiangazi.

Mchezaji huyo wa kimaita wa Colombia anapendelea kuondoka Real Madrid mwishoni mwa msimu, kwa mujibu wa AS.

Hata hivyo, magazeti ya Hispania yalidai miamba hiyo ya ‘La Liga’ wasingependelea kuondoka kwake kwa bei yoyote huku mabosi wote wawili, rais Florentino Perez na kocha Zinedine Zidane wakitaka kuendelea nae na kumsaidia kurudisha upya kiwango chake cha ubora.

Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 24 alifurahia mwanzo mwema hapo Santiago Bernabeu chini ya Carlo Ancelotti kufuatia uhamisho wake wa euro milioni 80 kutoka Monaco majira ya kiangazi ya mwaka 2014.

Mchezaji huyo ambaye alikuwa mmoja wa nyota waliotamba kwenye fainali za Kombe la Dunia mwaka 2014, alitua katika kikosi cha “Los Blancos” kujaza nafasi iliyokuwa imeachwa na Angel Di Maria.

Kwa Real Madrid ilikuwa ni kuimarisha matarajio kutoka msimu wake wa kwanza, baada ya kufunga magoli 17 na kutoa pasi 18 katika mechi 46.

Lakini James alishindwa kupata mafanikio katika msimu wake wa pili katika La Liga chini ya kocha wa zamani, Rafa Benitez na mrithi wake, Zidane. 

Alianza mechi 17 tu za La Liga msimu huu na zaidi ya tatu katika Ligi ya Mabingwa Ulaya na kufunga magoli manane na kuanzisha pasi 10 katika mchakato huo.

James amekuwa akipuuzwa na Zidane katika mechi kubwa za hivi karibuni, kama Ligi ya Mabingwa Ulaya mara mbili dhidi ya Manchester City au katika “El Clasico” dhidi ya Barcelona katika La Liga baada ya kuanguka katika utaratibu wa kupanga wachezaji.

AS lilidai katika ukurasa wa mbele kuwa Mcolombia huyo hakufurahishwa na ukosefu wake wa fursa ya kucheza na akiangalia kuondoka katika klabu hiyo mwishoni mwa msimu. 

Ripoti hiyo ilidai kuwa nyota huyo wa zamani wa Monaco na Porto ataitisha mkutano na wakurugenzi wa klabu baada ya fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya hapo Mei 28, ili kujadili kuondoka kwake.

NIGGAR ONE KUACHIA KICHUPA CHA “AMAELA” KESHO

$
0
0


MKALI wa Bongofleva anayefanya shughuli zake za muziki Tanzania na Uganda, Swaib Rashid “Niggar One”, kesho anatarajia kuachia “kichupa” cha wimbo wake mpya uitwao “Amaela”.

Akiongea na Saluti5, Niggar One amesema kwamba Amaela ni kibao kilichobeba meseji kali juu ya maisha ya utafutaji pesa.

Amesema kuwa, picha za video ya kibao hicho kilichopo katika miondoko ya Chakacha zimechukuliwa na Director mahiri aitwaye Pablo.

Niggar One amesema anaamini kichupa hicho kitawavuta mashabiki wengi kutokana na namna kilivyoandaliwa kwa umakini mkubwa kwa kuzingatia matakwa ya mashabiki na wakati wa sasa.

“Nawaomba mashabiki wanipe sapoti ya kutosha kwenye video hiyo ambayo baadhi ya picha zake zimechukuliwa maeneo muhimu kama vile daraja jipya la Nyerere, Kigamboni,” amesema.

ROBERT LEWNDOWSKI KUIKACHA BUNDESLIGA MWISHO WA MSIMU HUU

$
0
0


STRAIKA Robert Lewndowski ameweka bayana dhamira ya kutaka kuachana na Bundesliga ifikapo mwishoni mwa msimu wa mwaka 2019.

Kauli hii inakuja siku chache tu baada ya kuwepo kwa tarifa kuwa bosi wake wa Bayern Munich, Jose “Pep” Guardiola tayari ametangaza kutua katika kikosi cha Manchester City ifikapo mwishoni mwa msimu huu.

Hata hivyo, kuna tetesi kuwa Lewndowski ana asilimia kubwa ya kumfuata bosi wake (Guardiola) katika klabu ya Manchester City na kwamba taarifa za hivi sasa kutangaza kuondoka Bayern ni mwanzo tu wa kukamilisha dili hilo.
City tayari imeweka bayana mkakati wa kutaka kumsainisha straika huyo ifikapo mwanzoni mwa msimu wa mwaka 2016 kwa dau la pauni 45 mil. 

Pep ambaye ni kocha wa mabingwa hao wa Ujerumani, ameshakamilisha mazungumzo na uongozi wa juu wa Manchester City na kukubaliana kila kitu kinachohusiana na maslahi ya kandarasi yake hiyo mpya.

Wakala wa Lewndowski, Cezary Kucharski, amenukuliwa akikiri kuwa tayari ametaarifiwa juu ya utayari wa kuondoka kwa straika huyo aliyetua Bayern akitokea Dortimund.

Kucharski alibainisha pia kuwa mchezaji huyo tayari ameonyesha nia ya kuhama kutoka Bundesliga na huenda akatua England au Hispania.

Taarifa za uwezekano wa kuhama kwa mpachika nyavu huyo zinakuja kufuatia gazeti la Telegraph kuanika tetesi za hivi karibuni za kutakiwa na klabu za Barcelona na Manchester United.

Akinukuliwa zaidi, wakala huyo alisema; “Ninafikiri inawezekana kuwa ni ofa ya hali ya juu kwake kuhama kutoka Bayern lakini haitakuwa chini ya euro 50 mil.”

“Robert ni kati ya wachezaji walio na thamani kubwa kwa sasa ambao wako sokoni kwa ajili ya msimu huu wa usajili wa majira ya kiangazi.”

“Kila timu inamtaka Robert kwa gharama inayofanana na hadhi aliyonayo, kwasababu ana uwezo mkubwa wa kufunga magoli hasa katika mazingira tofauti.”

“Thamani yake hupanda kadri miaka inavyokwenda, kwavile yuko katika kiwango cha juu kwani ana wastani mzuri wa kupachika mabao nyavuni.”
“Ukiwana mchezaji wa hadhi ya Robert unaweza ukajivunia kuwa na kikosi cha ushindi na ninaamini anaweza kwenda katika Ligi kama ya England ama ya Hispania lakini kwa kukubali ofa wanayoitaka Bayern Munich,” alisisitiza wakala huyo.

LEICESTER CITY WAFANIKIWA KUMZUIA JAMIE VARDY

$
0
0


 VINARA wa Ligi ya Premier, Leicester City, ni kama walikuwa wanapigana katika mambo mawili; kutwaa ubingwa na kumbakiza straika wao mahiri, Jamie Vardy na sasa wamefanikiwa katika masuala yote mawili.

Wakati ambapo tayari wameshafanikiwa kutwaa ubingwa wa Premier msimu huu, uongozi wa machampioni hao tayari umefanikiwa pia kumshawishi straika huyo kuongeza kandarasi mpya juu ya ile ya kwanza ya miaka mitatu juu ya mkataba wake wa sasa ambao ulikuwa unamalizika 2017.

Kwa mkataba wa sasa, Vardy atalazimika kubaki katika kikosi cha Lecester City kwa miaka mitatu mingine na sasa atamaliza kandarasi yake mnamo mwaka 2020.

Awali Vardy alikuwa anaendelea na mazungumzo na bosi wa Leicester City Claudio Ranieri kabla ya kipindi cha kuelekea sikukuu ya Krismasi na mwaka mpya juu ya hatua hiyo ya dili hilo.

Akizungumzia kandarasi hiyo mpya, Vardy alisema kwa sasa suala lililo mbele yake sio idadi ya miaka ya kubaki katika klabu hiyo bali ni kukamilika kwa ndoto yao ya kuwa vinara na kisha kutwaa ubingwa wa premier.

Mchezaji huyo wa zamani wa Fleetwod Town alisema: “Nina furaha kuona bado tunaendelea kupambana kwa ajili ya klabu, sikutarajia tangu mwanzo kama tutafika hapa tulipo.”

“Kwa ajili hii, ninajivunia kuwa hapa kwa kipindi kirefu, ninataka kuwa ehemu ya mafanikio haya ambayo tumeyaanza msimu huu.”

“Leicester City ilionyesha haikuwa na madhara wakati nikiwasli hapa miaka mitatu iliyopita. Ni ngumu kupima mafanikio haya kwa muda huu, lakini inanifanya nione kuwa jambo limefanywa nami nikiwa sehemu ya hayo yote.”

“Ninafarijika na uwekezaji huu wa klabu ambao umenifanya niwe mtu wa kuitumikia kwa nguvu zangu zote kama sehemu ya kulipa fadhila kwa kufanya kazi maradufu,” amesisitiza Vardy.
Katika hatua nyingine, Vardy ameongezwa kitita cha mshahara wake wa juma kutoka ule wa awali ambao alikuwa analipwa 45,000 kwa wiki, lakini hata hivyo klabu yake hiyo ilikataa kuweka bayana zaidi ya kukiri kuwa ataingia katika orodha ya wanandinga wanaolipwa mshahara mnono.

MATIAS KRANEVITTER AKIRI KUGOMBEWA NATIMU ZA PREMIER

$
0
0


NYOTA wa Atletico Madrid, Matias Kranevitter amekiri tetesi za kuwaniwa na timu kadhaa za premier, lakini Chelsea na Manchester City ndio wanaongoza mbio hizo.

Lakini matajiri wa jiji la London, Chelsea wameongeza kasi ya kumwania kiungo mwenye umri wa miaka 22 kwa ajili ya kutua darajani katika usajili wa majira ya kiangazi.

Awali Kranevitter amekuwa akihusishwa na tetesi za kutaka kutua kwa washika Mitutu wa jiji la London na Arsene Wenger ameweka mezani ofa kwa ajili yake.

Lakini kocha wa sasa wa mpito wa matajili hao, Guus Hiddink inasemekana ameingilia kati dili hilo na anapambana kuhakikisha kiungo huyo anatua katika kikosi cha Stanford Bridge.

Akinukuliwa kiungo uyo amesema, ndoto zake za kutua Emirates zinaweza kuyeyuka kwa sababu Hiddink ameongeza kasi ya mazungumzo.

“Nimekuwa nikisikia malengo ya Hiddink kwangu na kadri ninavyotambua mpango upo hivyo.”

“Ni kati ya makocha wazuri duniani wanaovutia kufanya kazi nao na kila mchezaji anaota ndoto ya kufundishwa na mwalimu wa mfano wake.”

“Kwa nyakati tofauti nimekuwa nikifundishwa na makocha wengine kama kuna siku inatokea Napata nafasi ya kufanya kazi chini yake nitakuwa na furaha kubwa.”

“Lakini kwa sasa bado nipo Atletico, najisikia furaha kuwa hapa, hakuna tatizo kuwavhapa.”

“Kucheza katika timu iniyoshiriki Ligi ya mabingwa ni kati ya malengo yangu, pia kila mchezaji anaota mafanikio kama hayo.”
 
“Ninatarajia kuwa katika kiwango hicho cha mafanikio, ninaamini kuwa siku nitafikia hatua hiyo, ni suala la kusubiri kuona,” alisisitiza Matias Kranevitter.

ALEX SANDRO ATHIBITISHA KUTAKA KUONDOKA JUVENTUS

$
0
0



ALEX Sandro tayari ameonyesha azma ya kutaka kuondoka Juventus ili akatafute maisha mbele ya safari katika usajili huu wa majira ya kiangazi.


Tena amekwenda mbali zaidi kwa kuitaja timu anayoipenda kwenda kukipiga na kwamba mapenzi yake ni kuvaa uzi wa Manchester City.


Mshambuliaji huyo ameuomba uongozi wa klabu ya Juve licha ya kumruhusu aondoke anataka kwenda kutimiza azma yake ya kucheza Ligi ya premier.


Sandro ambaye msimu huu amekuwa katika kiwango bora akiwa na Juve lakini ameweka bayana ndoto yake ya kucheza katika Ligi iliyo na mashabiki wengi.


“Nina malengo ya kutimiza ndoto ya kwenda kucheza katika Ligi ya premier.”


“Ninataka kuona ninalinda kipaji change, sitaki kuwa msiri wa juu ya mimi kuondoka hapa.”


“Soka ni kazi ninayokwenda kufanya popote, soka ni mchezo wa kuangalia leo na kesho, huu ndio msimamo wangu kwa sasa,” alisema Sandro.

“Manchester City ni klabu ninayoipenda kwa ajili ya soka langu la baadae, naamini nina nafasi ya kucheza nikiwa kule na kutimiza ndoto yangu hii,” alisisitiza Sandro raia wa Brazil.

CARLO ANCELOTTI AMTUPA SOKONI MARIO GOTZE

$
0
0



KOCHA wa klabu bingwa Ujerumani, FC Bayern Munich, Carlo Ancelotti amekubali kumweka sokoni kiungo mshambuliaji Mario Gotze kwa kutaja thamani ya ada yake ya uhamisho kuwa pauni mil. 35.

Chelsea walitangulia katika mpango wa kutaka kumsajili kiungo huyo aliyeipa ubingwa wa dunia timu ya taifa ya Ujerumani kwa kufunga bao la ushindi dhidi ya Argentina mwaka 2014 kule nchini Brazil.

Ancelotti ambaye aliwahi kufanyakazi huko Stanford Bridge, anaamini thamani ya pauni mil. 35 inawezekana kwa kiungo huyo na huenda ikawa rahisi kwa klabu ya Chelsea kumsajili na kutimiza malengo yake chini ya utawala wa meneja Antonio Conte.

The Blues wameripotiwa kutenga kiasi cha pauni mil. 100 ambazo zitatumika katika mipango ya kufumuana kukisuka upya kikosi chao ambacho kwamsimu huu hakikufanya vyema.

Meneja Antonio Conte ameshahakikishiwa uwepo wa fedha hizo na ametakiwa kufanya kazi ya usajili ambao utamsaidia katika hatua ya kurejesha heshima huko magharibi ya jiji la London.

Hata hivyo Gotze anatajwa kuwa katika rada za aliyewahi kuwa bosi wake wakati akiwa na klabu ya Borussia Dortimund, Jurgen Klopp ambaye kwa sasa anatoa huduma ya ukufunzi nchini England akiwa na klabu ya Liverpool.

Kwa mantiki hiyo, inadhihirisha kwamba thamani ya Gotze pia itawahusu majogoo wa jiji kama kweli watakuwa na mipango ya kumsajili.
 
Klopp anaamini kama atafanikiwa kumnasa Gotz kikosi chake kitaimarika maradufu kwa msimu ujao wa Ligi nchini England ambao umeshatabiriwa kuwa na mshikemshike mkali.

BLACY CHYNA ANASA UJAUZITO WA ROB KARDASHIAN

$
0
0



CHUNGU imegeuka tamu kwa mwanadada Blacy Chyna (27), bada ya kunasa ujauzito wa kijana Rob Kardashian (29), ambaye alikuwa anapigwa vita na familia yake aachane na mrembo huyo.

Chyna alifunguka hivi karibuni kupitia mtandao wa Hollywoodlife.com akisema mekuwa raha kwake kupata ujauzito pia yupo kwenye maandalizi ya kufunga ndoa na Rob.

Hata hivyo baadhi ya mashabiki waliishambulia familia ya Rob kwa kitendo cha kutaka kuvunja uhusiano wa wawili hao.
 
Licha ya madongo yanayoikumba familia ya The Kardashian, iliamua kupokea taarifa hiyo ya ujauzito kwa furaha baada ya kupiga picha ya pamoja na mwanadada huyo kasha kuisambaza kwenye mitandao.

"UNGA" WAMPAGAWISHA JUSTIN BIEBER

$
0
0


NYOTA wa muziki wa Pop, Justin Bieber anaonekana kupagawishwa na dawa za kulevya “unga” baada ya kuanza kutembea pekupeku, kibaya ni kwamba anasema hatapiga picha za “selfie” na shabiki yeyote.

Bieber ambaye hivi karibuni alilazimika kulipa dola laki moja kwa sabau ya kuvunja simu ya shabiki wake aliyempiga picha, amezidi kuwashangaza mashabiki wake.

Alianza kwa kukataa kuwasalimia mashabiki kila anapomaliza onesho kama ilivyo ada lakini sasa anakuja na hiyo kali ambapo mashabiki wanasema wanahisi ni kutokana na utumiaji wa madawa ya kulevya.

Teja huyo tayari ameachana na mpenzi wake, Selena Gomez na ameapa kupitia mtandao wake wa Twitter akisema: “Najua kwamba watu hawatafurahia lakini hakuna mtu anayenidai picha.”

Katika ujumbe huo ambao Bieber aliambatanisha na picha alizokuwa akitembea peku katika mbuga moja jijini Boston, alisema : “Iwapo utakutana nami mahali ujue kwamba sitapiga picha tena.”
 
Hata hivyo baadhi ya mashabiki wamesema huo ni mfumo mbaya wa mwanamuziki huyo kijana kwani anaonekana amelanduka.
Viewing all 8805 articles
Browse latest View live
<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>