CRISTIANO RONALDO ameibua upya uwezekano wake wa kurejea England na kucheza katika Premier League baada ya kukwazwa na suala lake la kodi ya mapato Hispania.
Mchezaji huyo wa zamani wa Manchester United amesema atafurahi kurejea England ingawa hamaanishi kuwa ni lazima arejee.
"Samaniishi kuwa lazima nirejee Premier League lakini sikuwahi kuwa na tatizo lolote England," alisema Ronaldo