KOCHA wa Yanga, George Lwandamina amesema kuwa mchezo wao wa pili wa Ligi kuu Tanzania Bara dhidi ya Njombe Mji wameupania na wamejipanga vizuri zaidi ili kuweza kuondoka na point zote tatu.
Kocha huyo raia wa Zambia amesema maandalizi yao yanakwenda vizuri kuhakikisha wanashinda mchezo huo ambao ni wa pili tangu kuanza kwa ligi hiyo msimu huu.
Hata hivyo Lwandamina amewaacha washambulkiaji wake, Amis Tambwe na beno kakolanya na baruani yahya ambao hawatasafiri kwa ajli ya mchezo kwani bado hawapo fiti.