KIUNGO wa kimataifa wa Hispania anayekipiga Arsenal, Sant Cazorla amedai kuwa angefurahi kupewa mkataba mpya na klabu hiyo.
Kauli ya nyota huyo mwenye umri wa miaka 31 inakuja huku kukiwa na taarifa kuwa anatakiwa na Atletico Madrid.
“Ninafurahia kuwa hapa. Naaminiwa na kocha na wachezaji wenzangu. Najiona ni mtu muhimu hapa na atanipa mkataba mpya,” alisema.