Quantcast
Channel: saluti5
Viewing all articles
Browse latest Browse all 8805

BADO POINTI 2 LEICESTER KUBEBA TAJI LA PREMIER LEAGUE ...MANCHESTER UNITED YACHELEWESHA SHANGWE ZA UBINGWA

$
0
0
Manchester United imechelewesha shangwe za ubingwa wa Ligi Kuu ya England kwa Leicester City baada ya  sare ya 1-1 ndani ya Old Trafford baina ya timu hizo mbili.

United ilikuwa ya kwanza kupata bao dakika ya 8 kupitia Anthony Martial lakini Leicester City ikazawazisha dakika 11 baadae mfungaji akiwa ni nahodha  Wes Morgan.

Kama Leicester City ingeshinda mchezo huo, basi moja kwa moja wangekuwa ni mabingwa wapya wa England, lakini kwa sare hiyo sasa klabu hiyo imebakiza pointi mbili tu kutoka kwenye michezo yao mitatu iliyobakia ili kutwaa ubingwa.

Kimahesabu klabu pekee inayoweza kufikia pointi 77 za Leicester City ni Tottenham yenye pointi 69 ambayo ili iwe bingwa, inapswa kushinda michezo yake yote na Leicester City ipoteze mechi zote.

Tottenham inacheza na Chelsea Jumatatu usiku na iwapo matokeo yatakuwa sare, basi Leicester City itajikuta ikichukua ubingwa nje ya uwanja.

Manchester United: De Gea, Valencia, Smalling, Blind, Rojo, Carrick, Lingard (Mata 61mins), Rooney, Fellaini (Herrera 74), Martial, Rashford (Depay 82)

Leicester: Schmeichel, Simpson, Morgan, Huth, Fuchs, Mahrez (King 88), Kante, Drinkwater, Schlupp (Albrighton 77), Okazaki (Gray 66), Ulloa
Leicester did not get the win they needed to confirm themselves as champions but took a point from Old Trafford on Sunday
Leicesteri imeshindwa kutwaa taji kwenye uwanja wa Old Trafford 
Wes Morgan yells towards the camera after scoring at Old Trafford as Leicester tried to win the title with a win
Wes Morgan akishangilia bao lake la kusawazsisha
Both goalscorers Anthony Martial (centre) and Morgan (right) acknowledge each other after full time at Old Trafford
Wafungaji wa mchezo huo Anthony Martial (katikati) na Morgan (kulia) wakipeana pongezi baada ya mchezo
Martial pictured scoring the opener for Manchester United after only eight minutes at Old Trafford
Martial akiifungia United
Martial runs away in celebration after scoring the first goal of the afternoon for Manchester United on Sunday
Martial anakimbia kushangilia goli lake
Martial made life difficult for Leicester as Manchester United took an early lead against the Premier League title chasers
Martial aliipa wakati mgumu Leicester wakati Manchester United ipotangulia kufunga


Viewing all articles
Browse latest Browse all 8805

Trending Articles



<script src="https://jsc.adskeeper.com/r/s/rssing.com.1596347.js" async> </script>